Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Uchaguzi wa wanawake Chadema waingiliwa
Habari za Siasa

Uchaguzi wa wanawake Chadema waingiliwa

Halima Mdee, aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha)
Spread the love
HALIMA James Mdee, mmoja watu “waliodekezwa” ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), hadi kujigeuza “mungu mtu,” anatajwa kutaka kujimilikisha baraza la wanawake la chama hicho (Bawacha). Anaripoti Mwandishi  Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa kutoka makao makuu ya chama hicho, Kinondoni, mkoani Dar es Salaam zinasema, Mdee amepanga kujimilikisha Bawacha, kupitia uchaguzi wake, unaotarajiwa kufanyika 7 Machi mwaka huu.

Uchaguzi mkuu wa Bawacha, unalenga kujaza nafasi zilizoachwa wazi na Mdee na wenzake, ambao walifukuzwa uanachama wa Chadema, Novemba mwaka jana.

Kwa mujibu wa vyanzo vya taarifa, Mdee ambaye alibebwa na mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, mithili ya “mtoto wa mwisho,” anapanga mkakati kuhakikisha kuwa viongozi wote watakaochaguliwa, ni “wafuasi wake.”

Kamati Kuu (CC) ya Chadema, iliyokutana Novemba mwaka jana, iliwafukuza uanachama Mdee na wenzake 18, kufuatia kupatikana na hatia ya usaliti, kuhujumu chama na kwenda bungeni kujiapisha kuwa wabunge.

Sharifa Suleiman, Makamu wa Bawacha-Zanzibar

Mbali na Mdee, wengine waliofukuzwa Chadema, ni pamoja na waliokuwa wajumbe wa Kamati Kuu, Ester Bulaya na Esther Matiko; aliyekuwa katibu mkuu wa Bawacha, Grace Tendega na aliyekuwa katibu mkuu wa Baraza la Vijana la chama hicho (Bavicha), Nusrat Hanje.

Wengine, ni aliyekuwa Makamu Mwenyekiti Bawacha (Bara), Hawa Mwaifunga; aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Bawacha (Bara), Jesca Kishoa; aliyekuwa katibu mwenezi wa baraza hilo, Agnesta Lambat na aliyekuwa mwenyekiti wa Chadema mkoani Mtwara, Tunza Malapo.

Katika orodha hiyo, wamo pia aliyekuwa naibu katibu mkuu wa Bawacha (Zanzibar), Asia Mwadin Mohamed; Cecilia Pareso, Naghenjwa Kaboyoka, Sophia Mwakagenda, Kunti Majala, Salome Makamba,  Anatropia Theonest, Conchesta Lwamlaza, Felister Njau na Stella Siyao.

Genge hilo lililopachikwa jina la Covid 19, limewasilisha rufaa Baraza Kuu (BKT), kupinga maamuzi hayo.

Hata hivyo, pamoja na Mdee na wenzake, kufutwa uanachama na wenyewe kupokea  adhabu hiyo kwa kukata rufaa, bado wameruhusiwa kuendelea kuwa wabunge, kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano.

Vyanzo vya taarifa vinasema, miongoni mwa mikakati aliojiwekea Mdee na genge lake, ni kuhakikisha Bawacha ambayo inaushawishi mkubwa kwa wanawake, inashindwa kutekeleza majukumu yake ya uhamasishaji kwa chama.

Amesema, kuna taarifa za kina kuwa Mdee na wenzake, wameweka wagombea wao na kwamba wanalenga kugharamia baadhi ya gharama za uchaguzi.

Miongoni mwa wanaotajwa kumrithi Mdee, ni mfuasi wake mmoja, aliyewahi kumleta makao makuu ya Bawacha na  kumfanya msaidizi wake.

Mfuasi huyo wa Mdee, amechukua fomu ya kuwania nafasi ya katibu mkuu. Alikuwa mmoja wa wafuasi wa Mdee, waliohudhuria msiba wa bibi yake, miezi miwili iliyopita.

MwanaHALISI Online, inaendelea kufuatilia hatua kwa hatua, minendo ya viongozi hao,  waliopewa kazi maalum na baadhi ya watu walioko kwenye mfumo kuhakikisha kuwa Chadema na hasa aliyekuwa mgombea wake wa urais, Tundu Lissu, wanadhoofika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!