Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Michezo Yanga kuwakosa nyota watano wakiivaa Coastal Union
Michezo

Yanga kuwakosa nyota watano wakiivaa Coastal Union

Cedric Kaze, Kocha wa Yanga
Spread the love

 

KOCHA wa Yanga, Cedric Kaze amesema atawakosa wachezaji watano kuelekea mchezo wa leo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Coastal Union. Anaripoti kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo wa mzunguko wa pili utapigwa kwenye Uwanja wa Mkwawani mkoani Tanga ambapo katika kipindi cha miaka mitano Yanga hawajawahi kuibuka na ushindi.

Akiongea na waandishi wa habari Kaze alisema kuwa kwenye mchezo wa leo atawakosa wachezaji watano kutokana na sababu tofauti huku malengo yao ya ushindi yakiendelea kusalia.

“Kwenye mchezo wa leo tutamkosa Mapinduzi Balama ambaye ni majeruhi ya muda mrefu, Carlinhos anatumikia adhabu, Said Ntibanzokiza bado hajapona pia tutamkosa Ditram Nchimbi ambaye aliumia kwenye mazoezi ya jana sambamba na Adeyum Salehe,” alisema Kaze.

Mchezo huo utapigwa majira ya saa 10 jioni huku Coastal Union wakiwa na kumbukumbu ya kupoteza kwa mabao matatu kwenye mchezo wa mzunguko wa kwanza uliopigwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!