Wednesday , 17 April 2024
Home Kitengo Michezo Yanga kuwakosa nyota watano wakiivaa Coastal Union
Michezo

Yanga kuwakosa nyota watano wakiivaa Coastal Union

Cedric Kaze, Kocha wa Yanga
Spread the love

 

KOCHA wa Yanga, Cedric Kaze amesema atawakosa wachezaji watano kuelekea mchezo wa leo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Coastal Union. Anaripoti kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo wa mzunguko wa pili utapigwa kwenye Uwanja wa Mkwawani mkoani Tanga ambapo katika kipindi cha miaka mitano Yanga hawajawahi kuibuka na ushindi.

Akiongea na waandishi wa habari Kaze alisema kuwa kwenye mchezo wa leo atawakosa wachezaji watano kutokana na sababu tofauti huku malengo yao ya ushindi yakiendelea kusalia.

“Kwenye mchezo wa leo tutamkosa Mapinduzi Balama ambaye ni majeruhi ya muda mrefu, Carlinhos anatumikia adhabu, Said Ntibanzokiza bado hajapona pia tutamkosa Ditram Nchimbi ambaye aliumia kwenye mazoezi ya jana sambamba na Adeyum Salehe,” alisema Kaze.

Mchezo huo utapigwa majira ya saa 10 jioni huku Coastal Union wakiwa na kumbukumbu ya kupoteza kwa mabao matatu kwenye mchezo wa mzunguko wa kwanza uliopigwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

Michezo

TFF, Amrouche ngoma nzito

Spread the loveVIPENGELE vya mkataba wa kazi aliotia saini Kocha Mkuu wa...

error: Content is protected !!