Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ubovu barabara Kigamboni: Tanroad, mkandarasi wapewa maagizo
Habari za Siasa

Ubovu barabara Kigamboni: Tanroad, mkandarasi wapewa maagizo

Spread the love

WAZIRI wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amemuagiza meneja wa Wakala wa barabara mkoa wa Dar es Salaam kufika katika barabara ya Gomvu – Kimbiji hadi Pembamnazi ili kuona hatua za kuchukua kutokana na ubovu wa barabara hiyo ulitokana na mvua zinazoendelea kunyesha. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Pia amemuagiza mkandarasi aliyepewa zabuni ya kujenga barabara ya Kibada – Mwasonga yenye urefu wa kilomita 41 kuendelea kukusanya vifaa vya ujenzi wa barabara hiyo wakati serikali ikijipanga kumpatia malipo ya awali kwa ajili ya kuanza kazi ya ujenzi wa barabara hiyo.

Bashungwa amebainisha hayo leo Jumatatu bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Kigamboni, Faustine Ndugulile (CCM) aliyehoji lini barabara ya Gomvu – Kimbiji – Pembamnazi itajengwa kwa kiwango cha lami.

Akijibu swali hilo, Bashungwa amesema barabara ya Gomvu – Kimbiji – Pembamnazi ni sehemu ya barabara ya Mjimwema – Kimbiji – Pembamnazi yenye urefu wa kilometa 49 ambayo inajengwa kwa awamu kwa kiwango cha lami kulingana na upatikanaji wa fedha.

Amesema kwa sehemu ya Cheka – Avic (km 2) tayari ujenzi umekamilika wakati kwa sehemu ya Avic – Kimbiji (km 10) taratibu za manunuzi ya kumpata Mkandarasi kwa ajili ya kuanza ujenzi zinaendelea.

“Aidha, ujenzi kwa sehemu iliyobaki ya Kimbiji hadi Pembamnazi itajengwa kulingana na upatikanaji wa fedha,” amesema.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!