SEKRETARIETI ya chama cha TLP imemchagua aliyekuwa Makamu Mwenyekiti Zanzibar, Hamadi Mkadamu kuwa kaimu mwenyekiti taifa wa chama hicho kufuatia kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti Agustino Mrema. Anaripoti Juliana Assenga, UDSM … (endelea).
Akizungumza mara baada ya uchaguzi huo uliofanyika leo tarehe 9 Septemba, 2022, makao makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa TLP, Richard Lyimo, Sekretarieti ya chama imewashindanisha Mkadamu na Makamu Mwenyekiti Taifa Bara, Dominata Rwechungura.
Katibu Mkuu amesema Sekretarieti ya chama ina jumla ya wajumbe kumi na waliohudhuria kikao hicho ni Makamu Mwenyekiti(zanzibar) Hamadi Mkadamu, Makamu Mwenyekiti(Rechengura,Naibu katibu Mkuu(zanzibar) Hussain Juma, Naibu katibu Mkuu Michael mrema, Naibu katibu Mkuu utawala Rwamugira.
Katibu Mkuu huyo amesema chama wamekutana na kuwapigia kura makamu wawili Dominata Rwechungnura(Bara) na Alhaji Hamadi Mkadamu(visiwani).
Amesema matokeo ya uchaguzi wa kati ya makamu hao wawili Hamad Mkadamu ndiye aliyeweza kuchaguliwa kushikilia nafasi hiyo ya uenyekiti taifa.
Richard pia amesema kwa kurejelea katiba ya TLP inayo mikutano mikuu miwili ambayo ni mkutano wa dharura na mkutano wa kikatiba.
Lyimo amesema kutokana na kutokuwepo kwa mwenyeketi chama kilishindwa kuitisha mikutano yake lakini mara baada ya kuwa amekwisha patikana Mwenyekiti wa muda watapanga ni lini kuita mkutano mkuu kwa ajili ya kumchagua rasmi mwenyekiti wa chama hicho.
Akizungumza mara baada ya kuchaguliwa Hamad amewashukuru wajumbe kwa kumchagua kukaimu nafasi hiyo mpaka pale atakapochaguliwa Mwenyekiti mwingine.
Hamad amesema kuwa atakuwa tayari kushirikiana na wajumbe wengine katika kuendeleza nyayo zake aliyekuwa mwenyekiti Agustino Mrema bila ya kwenda kinyume.
Leave a comment