TETEMEKO la ardhi lililotokea nchini China maeneo ya Kaskazini-Magharibi, limesababisha vifo vya watu zaidi ya 100 na kujeruhi 397. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).
Kwa mujibu wa mtandao wa BBC Swahili, tetemeko hilo limetokea usiku wa kuamkia leo Jumanne, likiwa na ukubwa wakipimo cha 5.9, lilipiga katika mikoa ya Gansu na Qinghai, nchini humo ambapo mbali ya kupoteza maisha ya watu, lilibomoa makazi.
Kufuatia tukio hilo, Rais wa China, Xi Jinping, ameagiza mamlaka za uokoaji zikatoe misaada katika maeneo yaliyoathirika.
Vyombo vya habari nchini China, vimeripoti kuwa idadi ya watu waliopoteza maisha imeongezeka hadi kufikia 118, wakati juhudi za kuwaokoa waathirika zikiendelea.
Watu takribani 20 hawajulikani na walipo, wakati 2,200 wakiokolewa huku maelfu wakikimbia makazi yao kwenda sehemu zilizo salama.
Wizara ya fedha ya China, imetenga Dola za Marekani 27.9 milioni, kwa ajili ya kushughulikia tukio hilo.
Leave a comment