Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo TECNO yagusa hisia: Mchezo wa hisani wachochea hamasa ya kuboresha viwanja vya jamii Afrika
Michezo

TECNO yagusa hisia: Mchezo wa hisani wachochea hamasa ya kuboresha viwanja vya jamii Afrika

Spread the love

 

KAMA mdhamini rasmi wa Kombe la  (AFCON) Afrika nchini Côte d’Ivoire, kampuni ya teknolojia , TECNO iliandaa mechi ya hisani iliyojaa nyota magwiji wa mpira wa miguu Africa siku ya pili ya sherehe ya ufunguzi. Mechi hiyo ilishirikisha Katibu Mkuu wa CAF, Véron Mosengo-Omba, wachezaji maarufu wa mpira akiwemo Jay-Jay Okocha, El Hadji Diouf, Asamoah Gyan, Dennis Oliech, na Erick Otieno, waliyoonyesha ushirikiano wao kwa michezo na maendeleo ya jamii.

Meneja Mkuu wa TECNO Akishikana Mkono na magwiji wa Soka Afrika

Picha ya pamoja Timu ya CAF Pamoja na magwiji wa Soka Africa

Kabla ya kuanza kwa mchezo wa kirafiki, TECNO ilitangaza mpango wa kufadhili matengenezo ya viwanja 100 vya mpira vya jamii zote Afrika ndani ya miaka mitano ijayo. Mpango huu unalenga kuhamasisha ushiriki wa vijana, kukuza maisha yenye afya, na kuhakikisha upatikanaji wa viwanja bora vya michezo katika jamii zisizopewa kipaumbele. Meneja Mkuu wa TECNO, Jack Guo, alisema kwa hamasa, “Tumeanzisha safari ya kuzitia mwangaza ndoto zisizohesabika kwa kuboresha viwanja 100 kote Afrika,” akisisitiza nguvu ya kubadilisha ya mpango wa TECNO. Taylan Tankpinou, mvulana wa miaka 10, aliongeza, “Asante kwa TECNO, tunajenga maeneo bora ya kuchezea na kukua!

Hotuba ya Mpango wa Kifadhili

Ili kuhamasisha zaidi, TECNO ilitangaza kwamba kwa kila goli lililofungwa katika mchezo huo liligharimu, dola $10,000 ambazo zingechangiwa kwenye kampeni hiyo. Mchezo ulimalizika na TECNO kuchangia dola $50,000 zaidi kwa mradi huo. Ahadi hii ilifanya kila goli kuwa shangwe si tu kwa wachezaji bali pia kwa vizazi vijavyo ambavyo vitafaidika na miundombinu bora.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!