MBUNGE wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Mussa Hassan Mussa Silima wa Jimbo la Amani Zanzibar (CCM) amefariki dunia leo tarehe 13 Oktoba, 2022 nyumbani kwake Zanzibar. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea).
Taarifa iliyotolewa na Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson imeeleza kuwa Ofisi ya Bunge kwa kushirikiana na familia ya marehemu inaratibu mipango ya mazishi na taarifa zaidi zitaendelea kutolewa.
“Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Mhe. Mussa Hassan Mussa. Natoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa, waheshimiwa wabunge na wananchi wa jimbo la Amani. Mwenyezi mungu awape moyo wa uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu,: amesema Spika Tulia.
Kwa mujibu wa taarifa za awali, mwili wa marehemu unapelekwa kijijini kwao Bwejuu kwa ajili ya maziko yanatarajiwa kufanyika saa kumi leo baada ya sala ya alasiri.
R.I.P mpendwa wetu,sote tu wasafiri