Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Shule ya Hazina kuendelea kuwa juu kitaaluma
Elimu

Shule ya Hazina kuendelea kuwa juu kitaaluma

Spread the love

SHULE ya Msingi Hazina imeahidi kuendelea kuwa juu kitaaluma kwa kuhakikisha inakuwa na walimu mahiri na wenye wito wa kazi ya ualimu. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Mkuu wa shule hiyo, Omari Juma wakati a mahafali ya shule hiyo yaliyofanyika mwishoni mwa wiki.

Alisema shule hiyo imekuwa mstari wa mbele kuhimiza elimu bora kwa kuwalea wanafunzi kimaadili na kuwapa ushauri unaowawezesha kuendelea kufanya vizuri kitaaluma.

Wanafunzi wa shule ya msingi Hazina wakiingia kwenye mahafali yao yaliyofanyia mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.

“Kwa kuzingatia kwamba dunia ya leo ni ya utandawazi ni jukumu letu kama walimu na walezi kuwaelimisha wanafunzi kuhusu kila wanachokifanya,” alisema

Alisema kwa miaka 17 tangu shule hiyo kuanzishwa imepata mafanikio makubwa kitaaluma kwani imekuwa na matokeo mazuri katika ngazi za wilaya, mkoa na hata kitaifa.

Alisema mwaka huu wameendelea kufanya vizuri na kufanikiwa kuwa shule ya kwanza kiwilaya na katika mkoa wamefanikiwa kuingia kwenye kundi la kwanza la ufaulu (band 1) .

Wanafunzi wa shule ya msingi Hazina wakionyesha bunifu mbalimbali kwenye mahafali hayo

“Katika ngazi ya taifa wanafunzi wetu wote wamefanikiwa kufaulu huku shule yetu ikifanikiwa kupata daraja A la ufaulu katika mtihani wa taifa wa mwaka 2022 na kwa mwaka huu tunatarajia matokeo makubwa zaidi,” alisema

“Pia tumefanikiwa kuibua vipaji mbalimbali vya watoto kama mlivyoona kwenye maonyesho na hii ni dalili nzuri kwamba katika maisha yao ya baadae wataendelea vizuri sana,” alisema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari Mchanganyiko

Ugawaji taulo za kike watajwa kutokomeza utoro shuleni

Spread the loveBAADHI ya wanafunzi na walimu wa shule za sekondari mkoani...

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

error: Content is protected !!