KATIBU wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam nchini Tanzania, Sheikh Issa Ponda na wenzake wanashikiliwa na jeshi la Polisi kwa kosa kuandamana kwa lengo la kushinikiza kusimamishwa kwa mapambano ya Israel na wapiganaji wa Hamas katika ukanda wa Gaza nchini Palestina. Anaripoti Faki Sosi …(endelea).
Sheikh Ponda na wenzake wanaokadiriwa kufika tisa wamekamatwa leo Ijumaa Mnazi mmoja walipapanga kuanza maandamano yao waliyolenga kufika mpaka Manzese Tip Top .
Maandamano hayo hayakufika popote baada ya kachero wa Jeshi la Polisi aliyevaa kiraia alipoonekana kumzuia Sheikh Ponda na wenzake kufanya maandamano hayo.
Kachero huyo alimtaka Sheikh Ponda aingie kwenye gari lao .
Kwa mujibu wa msaidizi wa Sheikh Ponda amesema kuwa kiongozi wao na wafuasi wengine tisa wapo kwenye mikono ya Polisi.
Kwani walivunja sheria gani? Lerngo lao lilikuwa ni sawa na la serikali. Katika Umoja wa Mataifa nchi yetu ilupiga kura ya kusimamisha mauaji ya Gaza. Na ndio lengo la Ponda. Sasa kosa liko wapi?