Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Sheikh Ponda awataka wanawake waislamu washiriki masuala ya kitaifa
Habari Mchanganyiko

Sheikh Ponda awataka wanawake waislamu washiriki masuala ya kitaifa

Spread the love

KATIBU wa Shura ya Maimsmu, Sheikh Ponda Issa Ponda, amewataka wanawake wa kiislamu washiriki katika masuala ya kitaifa ikiwemo ujenzi wa Maendeleo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Sheikh Ponda ametoa wito huo leo tarehe 16 Septemba 2023, katika Baraza Kuu la Wanawake wa Kiislamu Tanzania, lililofanyika jijini Dar es Salaam.

“Nawashauru mshirki katika masuala ya Maendeleo ya nchi, tumeelezwa rekodi zetu hazionyeshi kama tunashiriki mambo yanayotuhusu nchi wanawake wa kiislamu hawaonekani kushiriki mambo ya nchi. Sababu mambo ya nchi yanaguda kwa namna moja au mbalimbali na kutoshriki maana yake unatoa nafasi watu washiriki Kwa niaba yako,” amesema Sheikh Ponda.

Kiongozi huyo wa dini amesema kuwa, kutokuwepo ushiriki wao wa kutosha katika masuala ya kitaifa ikiwemo vikao vya maamuzi, kunasababisha maslahi yao kutolindwa.

Aidha, Sheikh Ponda amesema kushiriki katika masuala ya uongozi sio dhambi.

“Tunaposhiriki masuala ya nchi unajitetea mwenyewe na usiposhiriki unamuachia mwingine kwenye nafasi ile ya maamuzi. Tunapofanya mikutano ya kitaifa mnatakuwa mshiriki,” amesema Sheikh Ponda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi wa wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu

Spread the love  KAMISHNA wa Polisi Utawala Menejimenti ya rasilimali watu, CP...

Habari Mchanganyiko

Vijana 400 waguswa na programu ya “Learning for Life” ya SBL

Spread the love  PROGRAMU ya “Learning for Life” imetimiza dhamira ya Serengeti...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

error: Content is protected !!