KATIBU wa Shura ya Maimsmu, Sheikh Ponda Issa Ponda, amewataka wanawake wa kiislamu washiriki katika masuala ya kitaifa ikiwemo ujenzi wa Maendeleo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).
Sheikh Ponda ametoa wito huo leo tarehe 16 Septemba 2023, katika Baraza Kuu la Wanawake wa Kiislamu Tanzania, lililofanyika jijini Dar es Salaam.
“Nawashauru mshirki katika masuala ya Maendeleo ya nchi, tumeelezwa rekodi zetu hazionyeshi kama tunashiriki mambo yanayotuhusu nchi wanawake wa kiislamu hawaonekani kushiriki mambo ya nchi. Sababu mambo ya nchi yanaguda kwa namna moja au mbalimbali na kutoshriki maana yake unatoa nafasi watu washiriki Kwa niaba yako,” amesema Sheikh Ponda.
Kiongozi huyo wa dini amesema kuwa, kutokuwepo ushiriki wao wa kutosha katika masuala ya kitaifa ikiwemo vikao vya maamuzi, kunasababisha maslahi yao kutolindwa.
Aidha, Sheikh Ponda amesema kushiriki katika masuala ya uongozi sio dhambi.
“Tunaposhiriki masuala ya nchi unajitetea mwenyewe na usiposhiriki unamuachia mwingine kwenye nafasi ile ya maamuzi. Tunapofanya mikutano ya kitaifa mnatakuwa mshiriki,” amesema Sheikh Ponda.
Leave a comment