RAIS Samia Suluhu Hassan ameipongeza Klabu ya Yanga licha ya kutolewa na Mamelodi Sundowns katika hatua ya robo fainali ya mashindano ya ligi ya Mabingwa wa Shirikisho la Soka Afrika. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Katika mchezo huo uliomalizika leo Ijumaa usiku, Yanga imeondolewa kwa mikwaju ya penalti 3-2 baada ya dakika zote 90 zilizopigwa katika uwanja wa Loftus Versfeld jijini Pretoria nchini Afrika Kusini timu za Mamelodi Sundowns na Yanga kutoka sare tasa.
Gumzo katika mchezo huo ulioishia dakika 90 kwa 0-0 kama ilivyokuwa kwenye uwanja wa Benjamini Mkapa wiki iliyopita, ni shuti la kiungo mshambuliaji wa Yanga, Stephanie Aziz Ki dakika ya 58 ambalo liligonga mwamba wa juu kwa ndani na kuvuka mstari wa chini ndani lakini teknolojia ya VAR ikainyima Yanga goli hilo.
“Kutokana na matukio ya mchezo huo, Rais Samia kupitia akaunti yake ya mtandao wa X ameandika hivi; Mchezo mzuri Yanga. Mmeonesha kiu na juhudi ya kuiletea heshima nchi yetu hadi kufikia hatua hii.
”Tunatarajia makubwa zaidi kutoka kwenu kwenye mashindano haya (Ligi ya Mabingwa ya Shirikisho la Soka Afrika) msimu ujao. Tutaendelea kuwaunga mkono na kuwapa motisha.”
YANGA WANATAKIWA KUKATA RUFAA, HAIWEZEKANI GOLI LA WAZI NAMNA ILE LIKATALIWE!! AU KWA VILE NI MALI YA MOTSEPE NINI? HAYA MATOKEO YALIKUWA YAMESHAPANGWA KABISA. ILA KUKAA KIMYA NI MAKOSA LAZIMA DUNIA IONE NA KAMA NI UDHAIFU WA KANUNI BASI ZIFANYIWE MAREKEBISHO!! HAIWEZEKANI MECHI MUHIMU KAMA HIYO GOLI LIKATALIWE KIRAHISI TU!