Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Ruto akubali kupatanishwa na Uhuru
Kimataifa

Ruto akubali kupatanishwa na Uhuru

Spread the love

 

NAIBU Rais wa Kenya, William Ruto amekubaliana na ombi la Maaskofu wa Kanisa Katoliki nchini humo la kumpatanisha na Rais Uhuru Kenyatta. Anaripoti Patricia Kighono – TUDARCo … (endelea). 

Kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation la nchini humo, mazungumzo ya Ruto na viongozi hao wa kidini yalifanyika nyumbani kwake eneo la Karen jijini Nairobi.

Ruto amesema yuko tayari na ana utashi wa kukutana na Rais Kenyatta. Pia amesema uhasama baina yake na rais ulisababishwa na ‘watu kutoka nje’ ambao walitaka kunufaika na serikali ambayo hawakuiunda.

Amesema makubaliano ya Machi 2018 yanayofahamika kama ‘handshak’ baina ya kiongozi wa chama cha upinzani cha ODM, Raila Odinga na Rais Kenyatta yalikuwa chanzo.

“Kuna watu tu wanafki, walikuja na kusema huyu Naibu Rais tumuweke kando kwanza, lakini mimi niko tayari wakati wowote bila masharti kukutana na Rais Uhuru,” amenukuliwa Ruto.

Mzozo baridi umekuwa ukiendelea baina ya kambi ya Rais Uhuru Kenyatta na ile ya Naibu Rais William Ruto baada ya makubaliano baina ya Rais Kenyatta na kiongozi mkongwe wa upinzani yaliyoitwa ‘Handshake’.

Upande wa Rais Kenyatta unadai kuwa ‘handshake’ ilihusu makubaliano ya kurejesha umoja miongoni mwa Wakenya na hivyo kukomesha ghasia za kikabila zinazoibuka hususani kila baada ya uchaguzi.

Hata hivyo, Ruto anadai kuwa hakuhusishwa katika makubaliano hayo, na amekuwa akitengwa na Kenyatta katika masuala mbalimbali ya kitaifa baada ya ‘Handshake.’

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!