Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Rais Samia awapa ujumbe watahiniwa kidato cha sita
Elimu

Rais Samia awapa ujumbe watahiniwa kidato cha sita

Wanafunzi wakifanya mtihani
Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan, amewataka kheri watahiniwa wa mtihani wa kumaliza kidato cha sita, huku akiwaahidi kwamba Serikali yake inaandaa mazingira Bora ya hatua zinazofusta ikiwemo vyuo vya ufundi, vya kati na elimu ya juu. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Samia ametoa ujumbe huo Jana Jumatatu, kupitia ukurasa wake wa Twitter, ambapo wahitimu hao wanatarajiwa kuanza mitihani kuanzia Leo tarehe 2 Mei 2023, Hadi mwishoni mwa mwezi huu.

Nawatakia kila la kheri wanangu wote mnaoanza mitihani yenu ya Kidato cha Sita kesho. Tunawategemea. Tunawaamini.

“Naamini mmejiandaa vyema kwa hatua hii muhimu kwenye safari yenu ya elimu, na nawaombea kwa Mwenyezi Mungu awape utulivu na siha njema mkahitimishe salama na kwa mafanikio,” ameandika Rais Samia na kuongeza:

“Serikali itaendelea kuhakikisha inaandaa mazingira bora katika safari yenu kuelekea hatua zifuatazo ikiwemo Vyuo vya Ufundi, Vyuo vya Kati na Vyuo vya Elimu ya Juu.”

Kwa mujibu wa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), jumla ya watahiniwa 106,956, wamesajiliwa kufanya mtihani wa mwisho wa kumaliza kidato cha sita, kuhu watahiniwa 8,906 wakisajikiwa kufanya mitihani ya mwisho ya kozi ya ualimu katika ngazi ya astashahada na cheti.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari Mchanganyiko

Chongolo aagiza TAKUKURU kuchunguza ujenzi wa bweni

Spread the loveMkuu wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amemuagiza Kamanda wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

Ugawaji taulo za kike watajwa kutokomeza utoro shuleni

Spread the loveBAADHI ya wanafunzi na walimu wa shule za sekondari mkoani...

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

error: Content is protected !!