Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Maisha Elimu Rais Samia awapa ujumbe watahiniwa kidato cha sita
Elimu

Rais Samia awapa ujumbe watahiniwa kidato cha sita

Wanafunzi wakifanya mtihani
Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan, amewataka kheri watahiniwa wa mtihani wa kumaliza kidato cha sita, huku akiwaahidi kwamba Serikali yake inaandaa mazingira Bora ya hatua zinazofusta ikiwemo vyuo vya ufundi, vya kati na elimu ya juu. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Samia ametoa ujumbe huo Jana Jumatatu, kupitia ukurasa wake wa Twitter, ambapo wahitimu hao wanatarajiwa kuanza mitihani kuanzia Leo tarehe 2 Mei 2023, Hadi mwishoni mwa mwezi huu.

Nawatakia kila la kheri wanangu wote mnaoanza mitihani yenu ya Kidato cha Sita kesho. Tunawategemea. Tunawaamini.

“Naamini mmejiandaa vyema kwa hatua hii muhimu kwenye safari yenu ya elimu, na nawaombea kwa Mwenyezi Mungu awape utulivu na siha njema mkahitimishe salama na kwa mafanikio,” ameandika Rais Samia na kuongeza:

“Serikali itaendelea kuhakikisha inaandaa mazingira bora katika safari yenu kuelekea hatua zifuatazo ikiwemo Vyuo vya Ufundi, Vyuo vya Kati na Vyuo vya Elimu ya Juu.”

Kwa mujibu wa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), jumla ya watahiniwa 106,956, wamesajiliwa kufanya mtihani wa mwisho wa kumaliza kidato cha sita, kuhu watahiniwa 8,906 wakisajikiwa kufanya mitihani ya mwisho ya kozi ya ualimu katika ngazi ya astashahada na cheti.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Elimu

Viwanda zaidi ya 200 kuonyesha bidhaa maonyesho ya TIMEXPO Dar

Spread the loveSHIRIKISHO la Wenye Viwanda Nchini (CTI) kwa kushirikiana na Mamlaka...

Elimu

Wazazi wa wanafunzi waliokosa nafasi vyuo vikuu waonyeshwa njia na GEL

Spread the loveWAKALA wa Elimu ya Vyuo Vikuu Nje ya Nchi, Global Education...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

Elimu

Green Acres kuwakatia bima wanafunzi wote

Spread the loveShule ya Green Acres imejipanga kufanya mambo makubwa kwa mwaka...

error: Content is protected !!