RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemuapisha Pereira Ame Silima (62) kuwa Balozi wa Tanzania nchini Comoro. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Silima ameapishwa leo Jumapili, tarehe 7 Novemba 2021, Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma kuchukua nafasi ya Sylvester Mabumba ambaye haijaelezwa amestaafu au atapangiwa majukumu mengine.
Amewahi kuwa Mbunge wa Chumbani visiwani Zanzibar. Aidha, akiwa mbunge alipata fursa kuhudumu nafasi ya naibu waziri wa mambo ya ndani na naibu waziri wa wizara ya fedha.
Katika uchaguzi mkuu uliopita wa Oktoba 2020, Silima alijitosa kwenye mbio za urais ndani ya chama tawala- Chama Cha Mapinduzi (CCM), Zanzibar kutaka kuchukua nafasi iliyokuwa inaachwa wazi na Dk. Ali Mohamed Shein.
Hata hivyo, mwisho wa kinyyng’anyiro hicho, Dk. Hussein Ali Mwinyi alipitishwa na Halmashauri Kuu ya CCM kupeperusha bendera ya chama hicho na baadaye kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika 27 na 28 Oktoba 2021, akashinda uchaguzi mkuu.
Leave a comment