KAMATI kuu maalum ya chama tawala nchini Tanzania- Chama Cha Mapinduzi (CCM), imekutana leo Jumapili, tarehe 7 Novemba 2021, Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Kikao hicho, kinaongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan.
Picha mbalimbali za mnato, zinawaonesha wajumbe wa kikao hicho wakiwemo makamu wawili wa mwenyekiti, Philip Mangula-bara na Dk. Ali Mohamed Shein- Zanzibar ni miongoni waliohudhuria.
Pia, Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi naye amehudhuria kikao hicho maalum.
Haijafahamika agenda ya kikao hicho cha kamati kuu kinajadili nini.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI TV, MwanaHALISI Online na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali.
Leave a comment