Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Biashara Rais Samia aipongeza Camel Oil kwa mradi wa bilioni Zanzibar
Biashara

Rais Samia aipongeza Camel Oil kwa mradi wa bilioni Zanzibar

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan ameipongeza  Kampuni ya Camel Oil kwa kufadhili ujenzi wa mradi wa kituo cha michezo cha kufurahisha watoto kuanzia miaka mitano hadi 18. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Mradi huo unaofadhiliwa na kampuni ya Camel Oil ya Tanzania, utagharimu zaidi ya Sh bilioni moja na itachukua hadi miezi 12 kukamilika.

Rais Samia ametoa pongezi hizo jana Jumatano Kizimkazi Visiwani Zanzibar wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi huo.

Rais Samia ameupongeza uongozi wa kampuni hiyo na kusema umekuwa mtekelezaji na si watu wa maneno.

Akizungumza katika uzinduzi huo Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Edha Abdallah amesema mradi huo utakapokamilika unatarajiwa kuwanufaisha wakazi wa Kibuteni, Kizimkazi, Kusini Unguja.

Amesema mbali ya eneo la kuchezea pia kutakuwa na kumbi za sherehe na sehemu za kupumzikia watu wazima.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Biashara

Mwezi wa kutoboa ni huu, cheza Keno Bonanza utusue Maisha

Spread the love MWEZI wa Oktoba wengi hupenda kuuita mwezi wakutoboa wakiwa...

Biashara

Wataalam Uganda wapewa darasa teknolojia mpya uchimbaji madini katika maonesho Geita

Spread the loveMAONESHO ya Teknolojia ya Madini yamezidi kuwa darasa kwa wadau...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

error: Content is protected !!