RAIS Samia Suluhu Hassan ameipongeza Kampuni ya Camel Oil kwa kufadhili ujenzi wa mradi wa kituo cha michezo cha kufurahisha watoto kuanzia miaka mitano hadi 18. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Mradi huo unaofadhiliwa na kampuni ya Camel Oil ya Tanzania, utagharimu zaidi ya Sh bilioni moja na itachukua hadi miezi 12 kukamilika.
Rais Samia ametoa pongezi hizo jana Jumatano Kizimkazi Visiwani Zanzibar wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi huo.
Rais Samia ameupongeza uongozi wa kampuni hiyo na kusema umekuwa mtekelezaji na si watu wa maneno.
Akizungumza katika uzinduzi huo Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Edha Abdallah amesema mradi huo utakapokamilika unatarajiwa kuwanufaisha wakazi wa Kibuteni, Kizimkazi, Kusini Unguja.
Amesema mbali ya eneo la kuchezea pia kutakuwa na kumbi za sherehe na sehemu za kupumzikia watu wazima.
Leave a comment