Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais mstaafu ahukumiwa miaka 4 jela
Kimataifa

Rais mstaafu ahukumiwa miaka 4 jela

Moncef Marzouki
Spread the love

Mahakama ya mjini Tunis imemhukumu rais wa zamani wa Tunisia, Moncef Marzouki kifungo cha miaka nane jela baada ya kupatikana na hatia kwa kutaka kuchochea fujo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Marzouki, ambaye alikuwa mkuu wa kwanza wa dola kuchaguliwa kwa njia ya demokrasia baada ya vuguvugu la mapinduzi katika nchi za kiarabu mwaka 2011, anaishi nchini Ufaransa na hakuwepo mahakamani wakati hukumu hiyo ilipotolewa.

Msemaji wa mahakama amesema hukumu hiyo imetolewa kuzingatia kauli zilizotolewa na Marzouki zinazojumuisha uchochezi katika hotuba aliyoitoa mjini Paris.

Mwaka 2021 Marzouki ambaye aliiongoza Tunisia kuanzia mwaka 2011 hadi 2014, alihukumiwa kifungo cha miaka minne jela kwa kutishia usalama wa taifa baada ya kuitaka Ufaransa isitishe msaada wake kwa rais wa Tunisia Kais Saied kwenye maandamano ya mjini Paris.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!