Wednesday , 8 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Raila Odinga ageukia muziki, aachia kibao
Kimataifa

Raila Odinga ageukia muziki, aachia kibao

Spread the love

 

WAKATI kampeni za kuelekea Uchaguzi Mkuu nchini Kenya zikiendelea kupamba moto, mmoja wa wagombea urais katika uchaguzi huo, Raila Odinga kutoka Chama cha ODM, ameachia kibao kinachokwenda kwa jina ‘Fire’, yaani moto. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Odinga ambaye ameshirikishwa na msanii Kelvin Kionko maarufu nchini humo kwa jina la Bahati, ameonekana akiitikia kwenye kiitikio (chorus) ya video hiyo ambayo tangu iachiwe mapema leo tarehe 7 Machi, 2022 tayari ina watazamaji, 52,000.

Katika kibao hicho, mbali na Odinga na Bahati pia kimewashirikisha wabunge na viongozi mbalimbali wa Serikali ya Kenya wakiwemo gavana wa kaunti ya Mombasa, Hassan Joho; Junet Mohammed, Alfred Mutua, Babu Owino na wengine.

Kwenye kibao hicho Bahati anaonekana akimsifia Odinga, akisema yeye ndiye kiongozi ambaye anaweza kuleta maendeleo katika taifa hilo na kubadilisha maisha ya vijana wengi ambao wamehangaika kwa muda mrefu bila kazi.

Kibao hicho kinalenga kumpigia kampeni na kuuza sera za kiongozi huyo wa muungano wa Azimio kuelekea Uchaguzi Mkuu wan chi hiyo unaotarajiwa kufanyika Agosti mwaka huu.

Katika kibao hicho pia Bahatia anasema kwamba Odinga ndiye anaweza kumaliza ufisadi nchini humo ambao umedumu kwa muda mrefu.

Ifahamike kwamba hiki ni kibao cha pili kwa Raila Odinga mwaka huu, kibao cha kwanza kilikuwa ni Leo ni leo akiwa amemshirikisha msanii Emanuel Musindi.

Mbali na Bahati, pia Msanii Willy Paul alikuwa ametangaza kuachia kibao na Raila ila bado hakijapakuliwa mitandaoni, huku mashabiki wakijiuliza iwapo anafanya kiki au lah!

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!