Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Prof. Mkenda avitaka vyuo vikuu Afrika kujikita katika tafiti
Elimu

Prof. Mkenda avitaka vyuo vikuu Afrika kujikita katika tafiti

Spread the love

WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania, Prof. Adolf Mkenda amevitaka vyuo vikuu barani Afrika, kujikita katika kufanya tafiti zitakazojibu changamoto za wananchi, pamoja na kuandaa wahitimu watakaokidhi matakwa ya soko la ajira. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Rai hiyo imetolewa leo tarehe 28 Novemba 2023, jijini Dar es Salaam, wakati akifungua kongamano la 14 la Wadhibiti Ubora wa Elimu ya Juu barani Afrika (AfriQAN).

“Chuo kikuu kazi yake sio tu kurithisha uelewa, lakini kuzalisha uelewa mpya kwa kufanya tafiti. Vyuo vijikite katika masuala ya utafiti hii itasaidia kupata majawbau ya matatizo ya jamii. Mfano tumekuwa na tatizo la Malarria Ulaya hakuna Malaria , tufanye utafiti kujua kwa nini wenzetu wameweza,” amesema Prof. Mkenda.

Katika hatua nyingine, Prof. Mkenda amezitaka taasisi za elimu ya juu, kuongeza udahili wa wanafunzi, huku akitoa angalizo kwamba ongezeko hilo liende sambamba na ubora wa elimu itakayotolewa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari Mchanganyiko

Ugawaji taulo za kike watajwa kutokomeza utoro shuleni

Spread the loveBAADHI ya wanafunzi na walimu wa shule za sekondari mkoani...

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

error: Content is protected !!