Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi yaanza uchunguzi tukio la kifo Mbezi Luis
Habari Mchanganyiko

Polisi yaanza uchunguzi tukio la kifo Mbezi Luis

Jumanne Muliro, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam
Spread the love

 

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limeanza uchunguzi wa tukio la kifo cha Felix Mgeni, anayedaiwa kuuawa kwa kupigwa na kitu chenye ncha kali kichwani. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Ijumaa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, SACP Jumanne Muliro.

“Jeshi la Polisi Kanda Maalum linachunguza tukio la kifo cha Mgeni (47), mkazi wa Kimara Temboni, anayedaiwa kuuawa huko maeneo ya Mbezi Luis usiku wa tarehe 14 Julai 2023. Mwili wa marehemu umekutwa kwenye gari aina ya Toyota Rav 4, huku ukiwa na jeraha kubwa kichwani,” amesema Kamanda Muliro.

Kamanda Muliro amesema uchunguzi unaofanyika ni pamoja na, kupeleleza baadhi ya vitu vilivyokutwa eneo la tukio, vingine vikiwa ni vya jinsia ya kike.

“Mwili umehifadhiwa Hospitali ya Mloganzila kwa uchunguzi zaidi na hatua zaidi za kisheria zitachukuliwa baada ya uchunguzi wa kina,” amesema Kamanda Muliro.,

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

error: Content is protected !!