KIONGOZI wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francisco, amemteua Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino, Tawi la Arusha, Padre Wolfgang Pisa, kuwa Askofu wa Jimbo la Lindi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).
Taarifa hiyo imetolewa leo Jumamosi, tarehe 9 Aprili 2022 na Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Father Charles Kitima.
“Ubalozi wa Baba Mtakatifu nchini Tanzania, unapenda kutaarifu kuwa, leo tarehe 9 Aprili 2022, Baba Mtakatifu Francisco amemeteua Padri Wolfgang Pisa, Ofm, Capuchin, kuwa Askofu wa Jimbo la Lindi. Askofu mteule kwa sasa ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino, tawi la arusha,” imesema taarifa ya Father Kitima.
Taarifa ya Father Kitima imesema, TEC inampongeza Askofu Mteule Wolfgang Pisa, kwa uteuzi huo.
Kwa mujibu wa taarifa ya Padri Richard A. Mjigwa, kutoka Vatican, Papa Francisco amemteua Padri Pisa kushika wadhifa huo, baada ya kuridhia ombi la Askofu Pius Ngonyani, la kung’atuka kwenye nafasi hiyo.
Leave a comment