Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko NMB yaimwagia msaada Machinga Dar
Habari Mchanganyiko

NMB yaimwagia msaada Machinga Dar

Spread the love

BENKI ya NMB nchini Tanzania imetoa msaada wa  viti 15, meza 10, kabati moja pamoja na viti vya wageni viwili kwa Shirikisho la Umoja wa Machinga Tanzania (SHIUMA). Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Msaada huo uliokabidhiwa na Mkuu wa Idara ya Bima wa Benki ya NMB, Martine Massawe kwa Mwenyekiti SHIUMA, Ernest Masanja ni maalum kwa ajili ya ofisi ndogo ya makao makuu ya shirikisho hilo jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Idara ya Bima wa Benki ya NMB, Martine Massawe (wa pili kulia), akimkabidhi Mwenyekiti wa Shirikisho la Umoja wa Machinga Tanzania (SHIUMA), Ernest Masanja, sehemu ya msaada wa viti 15, meza 10, kabati 1 pamoja na viti vya wageni 2 vilivyotolewa na NMB kwa ajili ya ofisi ndogo ya makao makuu ya shirikisho hilo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti SHIUMA Taifa, Stephen Lusinde na kulia ni Mkurugenzi anayeratibu Makundi Maalum (Machinga) kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Juma Samwel.

Katika makabidhiano hayo pia alikuwepo, Makamu Mwenyekiti wa SHIUMA, Taifa, Stephen Lusinde na Mkurugenzi anayeratibu Makundi Maalum (Machinga) kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Juma Samwel.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

error: Content is protected !!