Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mwanamke ajifungua watoto saba, madaktari wapigwa butwaa
Kimataifa

Mwanamke ajifungua watoto saba, madaktari wapigwa butwaa

Spread the love

 

NI MIUJIZA! Ndivyo unavyoweza kueleza tukio la Mwanamke mmoja aliyejifungua watoto saba kwa mpigo mjini Abbottabad huko nchini Pakistan. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Tukio hilo limetokea juzi tarehe 17 Oktoba, 2021 katika mji wa Abbottabad nchini Pakistan baada ya mwanamke huyo aliyedhaniwa kuwa na ujaunzito wa watoto watano, kujifungua watoto saba.

Akizungumza na waandishi wa habari, mume wa mwanamke huyo, Yar Mohammad amesema Mungu amewajaalia watoto wanne wa kiume na watatu wa kike.

Amesema mkewe aliyejifungua katika Hospitali ya Kimataifa ya Jinnah, hali yake na watoto imeimarika na wanaendelea vizuri.

Mohammed amesema uchunguzi wa awali ulipobaini mke wake amebeba watoto kadhaa tumboni walishauriwa waende hospitali kubwa kwa uangaalizi wa karibu.

Ameongeza madaktari waliomhudumia walishangazwa sana hali ya mkewe.

Aidha, Mmoja wa madaktari bingwa walioongoza jopo la kumfanyia operesheni mwanamke huyo, Dk Hina Fayaz ambaye ni daktari bingwa wa wanawake katika Hospitali hiyo ya Jinnah, amesema mwanamke huyo alifika hospitalini hapo kwa mara ya kwanza Jumamosi tarehe 16 Oktoba mwaka huu.

“Baada ya uchunguzi wa ultrasound na ripoti zingine, tuligundua kuwa ana watoto watano ndani ya tumbo lake na ujauzito wake ulikua wa zaidi ya miezi minane.

“Tulishtuka sana kuona ripoti ya matibabu ya mwanamke huyu.

“Alikuwa na shinikizo la damu iliyotajwa kuwa ya kiwango hatari. Tumbo lake lilikuwa limevimba. Katika uzao wake wa kwanza na wa pili, alikuwa amejifungua watoto wawili kwa njia ya upasuaji, hivyo alikuwa na maumivu makali kwenye kovu la upasuaji wa kwanza,” amesema.

Amesema ni maajabu kuona mama huyo na watoto wake wote wametoka salama.

Aidha, kwa kuwa imelazimu mama huyo kufanyiwa upasuaji na kutolewa watoto hao waliokuwa na umri wa miezi nane kwa maana ya njiti, imebidi wawekwe kwenye chumba maalumu cha uangalizi kwa siku kadhaa kabla ya kuruhusiwa kutoka hospitali.

Hata hivyo, akizungumzia sababu za mwanamke kubeba ujauzito wa mapacha wengi kiasi hicho, Dk. Fayaz amesema sababu kubwa ni matumizi ya dawa za kuchagiza upatikanaji wa ujauzito kupita kiasi.

“Ndio maana huwa tunashauri matumizi ya dawa hizi yatolewe na daktari mwenye ujuzi wa kutosha ili kuokoa maisha ya mama anayehitaji mtoto,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!