JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, kinamshikilia mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Qiblaten Kawe, Mohamed Jabir, kwa tuhuma za kumuua Mwalimu wake, Hassan Mohamed. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).
Akizungumza na waandishi wa Habari Leo Ijumaa, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, SACP Jumanne Muliro, amesema tukio Hilo limetokea alfajiri ya tarehe 20 Julai 2023.
Ni naada ya Jabiri kudaiwa kumchoma kwa kisu Mwalimu wake maeneo ya shingoni kitendo kilichopelekea kupoteza maisha.
“Mtuhumiwa alitekeleza kauaji hayo saa 11.10 alfajiri baada ya kumshambuliwa Mwalimu (Patron), aliyekuwa akiwahimiza wanafunzi wakati wa kuhudhuria ibada ya alfajiri. Majeruhi alifariki wakati anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala na mwili wake umehifadhiwa hospitalini hapo,” amesema Kamanda Muliro.
Kamanda Muliro amesema mtuhumiwa atafaikishwa Mahakamani haraka iwezekanavyo kwa hatua zaidi za kisheria.
Leave a comment