Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mlipuko wa bomu waua 50 katika sherehe za Maulidi ya Mtume
Kimataifa

Mlipuko wa bomu waua 50 katika sherehe za Maulidi ya Mtume

Spread the love

WATU takribani 50 wamefariki dunia huku wengine 50 wakijeruhiwa katika mlipuko wa bomu uliotokea karibu na msikiti nchini Pakistan, wakati wakisherehekea sikukuu ya maulidi ya kumbukumbu ya kuzaliwa Mtume Muhammad. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Kwa mujibu wa mtandao wa BBC Swahili, Jeshi la Polisi nchini humo limetaja chanzo cha mlipuko huo ni tukio la kujitoa mhanga lililolengwa katika mkusanyiko wa kidini.

Kufuatia tukio hilo lililotokea katika mji wa Mastung leo Ijumaa, vyombo vya usalama Pakistan, vimetangaza hali ya hatari.

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Pakistan, Sarfraz Bugti, amelaani tukio hilo akisema ni la kuchukiza.

Mitandao ya kimataifa imeripoti kuwa, Naibu  Inspekta wa Polisi wa Pakistan, Munir Ahmed, amedai mlipuaji bomu alilitekeleza tukio hilo karibu na gari ya polisi.

Imeelezwa kuwa, hadi sasa hakuna kikundi cha kigaidi kinachohusishwa na tukio hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!