Saturday , 2 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Mlipuko wa bomu waua 50 katika sherehe za Maulidi ya Mtume
Kimataifa

Mlipuko wa bomu waua 50 katika sherehe za Maulidi ya Mtume

Spread the love

WATU takribani 50 wamefariki dunia huku wengine 50 wakijeruhiwa katika mlipuko wa bomu uliotokea karibu na msikiti nchini Pakistan, wakati wakisherehekea sikukuu ya maulidi ya kumbukumbu ya kuzaliwa Mtume Muhammad. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Kwa mujibu wa mtandao wa BBC Swahili, Jeshi la Polisi nchini humo limetaja chanzo cha mlipuko huo ni tukio la kujitoa mhanga lililolengwa katika mkusanyiko wa kidini.

Kufuatia tukio hilo lililotokea katika mji wa Mastung leo Ijumaa, vyombo vya usalama Pakistan, vimetangaza hali ya hatari.

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Pakistan, Sarfraz Bugti, amelaani tukio hilo akisema ni la kuchukiza.

Mitandao ya kimataifa imeripoti kuwa, Naibu  Inspekta wa Polisi wa Pakistan, Munir Ahmed, amedai mlipuaji bomu alilitekeleza tukio hilo karibu na gari ya polisi.

Imeelezwa kuwa, hadi sasa hakuna kikundi cha kigaidi kinachohusishwa na tukio hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

Kimataifa

Papa Francis kumfukuza Kardinali anayepinga mageuzi Kanisa Katoliki

Spread the loveKIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, anadaiwa kupanga kumfumkuza...

Kimataifa

Mateka wa Israel, Gaza kuanza kuachiwa leo

Spread the loveMakubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Israel na vikosi vya...

Kimataifa

Israel, Hamas kusitisha mapigano kwa muda

Spread the loveNCHI ya Israel, pamoja na kikundi cha wanamgambo wa kiislamu,...

error: Content is protected !!