RAIS wa Urusi, Vladimir Putin, amefungua milango ya ushirikiano kwa vikundi vya kijeshi vya kujitolea ,ili kuongeza nguvu katika vita kati yake na Ukraine. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).
Ripoti hiyo imetolewa na Andrei Troshev, msaidizi wa zamani wa aliyekuwa kiongozi wa Kundi la Wagner, Yevgeny Prigozhin, aliyefariki dunia kwa ajali ya ndege miezi michache baada ya kutangaza uasi dhidi ya Serikali ya Putin.
Mtandao wa BBC Swahili umeripoti kuwa, Putin alitangaza uamuzi wa kushirikiana na vikundi vya kujitolea katika vita nchini Ukraine, wakati akizungumza na Troshev.
Troshev alisema Putin ameahidi kushirikiana na vikundi hivyo katika operesheni mbalimbali za kijeshi “unajua masuala ambayo yanahitaji kutatuliwa mapema ili mipangilio katika eneo la mapigano iende kwa njia bora na yenye mafanikio.”
Msemaji wa Serikali ya Urusi, Dmitry Peskov, alisema Troshev ambaye zamani alikuwa katika kundi la Wagner, amepewa nafasi katika Wizara ya Ulinzi.
Hayo yanajiri ikiwa umepita mwezi mmoja tangu Putin atoe wito kwa wanajeshi wa Wagner na wa vikundi vingine binafsi kula kiapo cha utii kwa Serikali yake.
Leave a comment