Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Putin aita vikundi vya kujitolea vita ya Ukraine
Kimataifa

Putin aita vikundi vya kujitolea vita ya Ukraine

Spread the love

RAIS wa Urusi, Vladimir Putin, amefungua milango ya ushirikiano kwa vikundi vya kijeshi vya kujitolea ,ili kuongeza nguvu katika vita kati yake na Ukraine. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Ripoti hiyo imetolewa na Andrei Troshev, msaidizi wa zamani wa aliyekuwa kiongozi wa Kundi la Wagner, Yevgeny Prigozhin, aliyefariki dunia kwa ajali ya ndege miezi michache baada ya kutangaza uasi dhidi ya Serikali ya Putin.

Mtandao wa BBC Swahili umeripoti kuwa, Putin alitangaza uamuzi wa kushirikiana na vikundi vya kujitolea katika vita nchini Ukraine, wakati akizungumza na Troshev.

Troshev alisema Putin ameahidi kushirikiana na vikundi hivyo katika operesheni mbalimbali za kijeshi “unajua masuala ambayo yanahitaji kutatuliwa mapema ili mipangilio katika eneo la mapigano iende kwa njia bora na yenye mafanikio.”

Msemaji wa Serikali ya Urusi, Dmitry Peskov, alisema Troshev ambaye zamani alikuwa katika kundi la Wagner, amepewa nafasi katika Wizara ya Ulinzi.

Hayo yanajiri ikiwa umepita mwezi mmoja tangu Putin atoe wito kwa wanajeshi wa Wagner na wa vikundi vingine binafsi kula kiapo cha utii kwa Serikali yake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!