Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Mfumuko wa bei wapaa
Habari Mchanganyiko

Mfumuko wa bei wapaa

Spread the love

MFUMKO wa bei umeongezeka kutoka asilimia 3.2 mwezi Aprili, hadi asilimia 3.5 mwezi Mei mwaka huu. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa Irenius Ruyobwa, Mkurugenzi wa shughuli za kitakwimu Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) amesema, kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwezi Mei imeongezeka ikilinganishwa na kasi iliyokuwepo Aprili mwaka huu.

Amesema, kuongezeka kwa mfumko huo kwa mwezi Mei, kumechangiwa na kuongezeka kwa bei za baadhi ya bidhaa za vyakula na bidhaa zisizo za vyakula kulinganisha na kipindi hiki mwaka 2018.

“Baadhi ya bidhaa za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa mfumko wa bei kwa kipindi hicho ni pamoja na unga wa mahindi, nyama, samaki, matunda, viazi na mihogo mibichi,” alisema Ruyobwa.

Na kuwa, bidhaa zisizo za vyakula zilizochangia ongezeko la mfumko wa bei wa taifa ni mavazi, viatu, mkaa, vyombo vya jikoni, gharama za kumuona daktari hospitaliti za binafsi, dizeli na petroli.

Pia amesema, mfumko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa kipindi cha mwezi Mei, umeongezeka hadi asilimia 2.2 kutoka asilimia 0.9 kwa mwezi April 2019.

Kuhusu hali ya mfumko bei kwa nchi za Afrika Mashariki amesema, Uganda mfumko wa bei kwa mwisho wa mwezi Mei 2019 umepungua hadi asilimia 3.3 kutoka asilimia 3.5 kwa mwezi Aprili mwaka huu.

Kwa upande wa Kenya mfumuko wa bei kwa mwezi Mei, 2019 umepungua hadi asilimia 5.9 kutoka asilimia 6.58 kwa mwezi Aprili mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi wa wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu

Spread the love  KAMISHNA wa Polisi Utawala Menejimenti ya rasilimali watu, CP...

Habari Mchanganyiko

Vijana 400 waguswa na programu ya “Learning for Life” ya SBL

Spread the love  PROGRAMU ya “Learning for Life” imetimiza dhamira ya Serengeti...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

error: Content is protected !!