KWA mara ya kwanza Halima Mdee na wenzake sita, ambao ni Wabunge wa Viti Maalum waliofukuzwa uanachama wa Chadema, wamefika mahakamani kuitika wito wa mahakama. Anaripoti Faki Sosi na Apaikunda Mosha, Dar es Salaam … (endelea).
Awali tarehe 29 Julai mwaka huu Mahakama hiyo ilikubali ombi la Mawakili wa Chadema lililowasilishwa na Peter Kibatala la kutaka waombaji saba kwenye kesi ya kupinga kuvuliwa uanachama wa Chadema, kufika mahakamani hapo.
Mdee na wenzake wameomba mahakama hiyo kutengua kuvuliwa kwa uanachama wao ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Shauri hilo limeanza kusikilizwa saa tano kamili ambapo Jaji Cyprian Mkeha ameanza kusikiliza pingamizi la upande wa waombaji .
Pingamizi hilo limewasilishwa kupinga kiapo kinzani cha upande wa wajibu maombi namba moja (Chadema).
Endelea kusoma MwanaHALISI Online kujua zaidi kinachoendelea mahakamani hapo
Leave a comment