SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Tulia Ackson ametangaza msiba wa Mbunge wa Kwahani, Ahmed Yahya Abdulwakil (CCM), aliyefariki dunia ghafla Visiwani Zanzibar. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Akitangaza msiba huo leo jioni bungeni jijini Dodoma, amesema Abdulwakil amefariki ghafla kutokana na matatizo ya shinikizo la damu.
Amesema kwa kuwa mwili wa mbunge huyo unatarajiwa kuzikwa kesho Jumanne shughuli za Bunge hazitokuwepo ili kutoa nafasi kwa wabunge kushiriki mazishi hayo lakini pia kwa kuwa Jumatano au Alhamis ni sikukuu ha Eid,hivyo anaahirisha Bunge hadi Jumatatu wiki ijayo.
Mbunge alifariki lini?