Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mateka wa Israel, Gaza kuanza kuachiwa leo
Kimataifa

Mateka wa Israel, Gaza kuanza kuachiwa leo

Spread the love

Makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Israel na vikosi vya Hamas yameanza leo Ijumaa saa moja asubuhi ikiwa ni mpango wa kusitisha mapigano kwa muda wa siku nne. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa …(endelea).

Kwa mujibu wa msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Qatar, ambayo inasaidia kujadili muafaka wa mapigano hayo, kundi la kwanza la mateka linatarajiwa kuachiliwa kutoka Gaza saa kumi jioni.

Msemaji huyo Majed Al-Ansari, aliwaambia waandishi wa habari jijini Doha kwamba usitishaji huo wa kwanza tangu vita kuanza mwezi uliopita utajumuisha usitishaji vita wa pande zote kaskazini na kusini mwa Gaza.

Kwa mujibu wa makubaliano hayo, wanawake na watoto 50 waliotekwa nyara kutoka Israel, na kundi la wanamgambo wa Hamas tarehe 7 Oktoba, 2023 wataachiliwa kwa kubadilishana na wanawake 150 wa Kipalestina na watoto wadogo waliofungwa gerezani nchini Israel.

Mateka 13 wataachiliwa kutoka Gaza leo saa 10 jioni na makundi mengine ya mateka yataachiliwa kila siku ya kusitisha mapigano hadi 50 waachiliwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!