MAPACHA wawili raia wa Japan, Umeno na Koume wenye miaka 107, wamevunja rekodi ya kuwa pacha wazee zaidi duniani. Anaripoti Noela Shila, TUDARCo … (endelea).
Kutokana na hilo, Umeno na Koume wameandikwakatika kitabu cha rekodi ya dunia ‘guinnes world record’ kama dada mapacha wanaofanana wakongwe duniani.
Kwa sasa, mapacha hao wana miaka 107 na siku 300 ambao walizaliwa tarehe 5 Novemba 1913 kwenye kisiwa cha Shodoshima, nchini Japan.
Awali, rekodi hiyo ilikuwa inashikiliwa na Kin na Gin, ambao walikuwa na miaka 107 na siku 175 hadi Kin alipofariki dunia Januari 2000.
Mwaka uliofuata yaani 2001, Gin alifariki dunia akiwa na miaka 108.
Mapacha hao, Kin na Gin ambao ssa ni marehemu, walizaliwa tarehe 1 Agosti 1892 huko Nagoya nchini Japan na walikuwa watu mashuhuri kwa vyombo vya habari katika kipindi cha muongo wao wa mwisho wa uhai.
Tuzo hizo zilitolewa jana Jumatatu tarehe 20 Septemba 2021, ambayo ilikuwa siku ya wazee duniani ambapo ni siku ya mapumziko ya kitaifa nchini mwao Japan.
Kutokana na ugonjwa wa korona (UVIKO-19) na tahadhari wadada hao mapacha wanaoishi sehemu tofauti za Japan walitumiwa vyeti vyao na wafanyakazi katika nyumba zao tofauti za utunzaji.
Leave a comment