Sunday , 5 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Makatibu wakuu wakagua ujenzi wa miundombinu Msomera
Habari Mchanganyiko

Makatibu wakuu wakagua ujenzi wa miundombinu Msomera

Spread the love

Makatibu wakuu wa wizara za kisekta leo ijumaa wametembelea kijiji cha Msomera  wilayani Handeni mkoani Tanga kujionea hatua mbalimbali za ujenzi wa miundombinu kabla ya kuanza kwa awamu ya pili ya kuhamisha wananchi wanaoishi  katika hifadhi ya Ngorongoro waliojiandikisha kuhama kwa hiari. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Wakiongozwa na Katibu mkuu ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia sera, Bunge na uratibu Dk. Jim Yonaz, makatibu wakuu hao wamekagua ujenzi wa miundombinu mbalimbali ikiwemo maji, umeme, madaraja,barabara, shule, nyumba za makazi na uboreshaji wa huduma za mawasiliano.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa zoezi hilo   mkuu wa wilaya ya Handeni mheshimiwa Albert Msando amesema vikosi kutoka SUMA JKT vinaendelea na kazi hiyo licha ya kuwepo kwa mvua nyingi.

Ameongeza kuwa awamu ya pili ya ujenzi huo  pamoja na miundombinu mingine unahusisha nyumba 5,000 ambapo nyumba 2500 ambapo zimefikia katika hatua mbalimbali za ujenzi.

Kwa upande wake Dk. Yonaz amemshukuru mkuu huyo wa wilaya kwa kushirikiana kwa karibu na watendaji mbalimbali katika kusimamia zoezi la ujenzi wa miundo mbinu.

Dk. Yonaz amesema serikali imejipanga katika kuhakikisha kuwa wizara zote za kisekta zinashiriki kikamilifu katika kuhakikisha kuwa mradi huo unakamilika kwa wakati ili kuwezesha wananchi wanaoendelea kujiandikisha kuhamia katika nyumba hizo.

Serikali inaendelea na zoezi la kuandikisha wanaonchi wanaohama kwa hiari  katika hifadhi ya Ngorongoro  na kuwapeleka katika maeneo mengine ili kulinda hifadhi na kuimarisha maisha ya wananchi nje ya eneo hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tanzania  yasisitiza kuwa Kituo Kikuu cha Uchimbaji Madini Afrika

Spread the loveTanzania imeendelea kusisitiza adhma yake ya kuwa kituo kikuu cha...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

error: Content is protected !!