Sunday , 5 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Somalia mwanachama mpya wa EAC
Habari za Siasa

Somalia mwanachama mpya wa EAC

Rais Hassan Sheikh Mohamud
Spread the love

JAMHURI ya Shirikisho la Somalia, imekubaliwa rasmi kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Uamuzi wa EAC kukubali ombi la uanachama wa Somalia, umetangazwa leo tarehe 24 Novemba 2023 na Mwenyekiti wa jumuiya hiyo anayemaliza muda wake, Evariste Ndayishimiye, katika mkutano wa 23 wa kawaida wa wakuu wa nchi za Afrika Mashariki, jijini Arusha.

Rais wa Somalia, Hassan Sheikh Mohamud, alikuwepo wakati Ndayishimiye ambaye ni Rais wa Burundi, anatangaza uamuzi huo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud kabla ya kuanza kwa Mkutano wa ndani wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) Ngurdoto Mkoani Arusha tarehe 24 Novemba 2023.

“Kuhusu maombi ya Jamhuri ya Shirikisho la Somalia, tumeamua kukubali ombi la Somali la kuwa mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki,” amesema Rais Ndayishimiye.

Ofisi ya Rais wa Somalia, kupitia ukurasa wake wa Twitter, mapema baada ya uamuzi huo kutangazwa, ilishukuru kwa taifa hilo kukubaliwa kujiunga katika jumuiya hiyo, huku ikiahidi kutoa ushirikiano kwa nchi wanachama katika kuleta ustawi na maendeleo.

“Ni siku ya kihistoria kwa Somalia katika mkutano wa 23 wa wakuu wa EAC mjini Arusha, Tanzania. Jamhuri ya Shirikisho la Somalia ina heshima kubwa ya kujiunga na jumuiya kama mwanachama wa nane, kuashiria enzi mpya ya matumaini na ustawi wa pamoja katika kanda,” imeandika ofisi hiyo.

Akizungumza baada ya uamuzi huo, Rais wa Kenya, William Ruto, aliipongeza Somalia kwa kuwa mwanachama, huku akisema EAC imeongeza idadi ya watu milioni 15.

“EAC tulikuwa saba sasa ziko nchi nane, mniruhusu kuipongeza Jamhuri ya Shirikisho la Somalia kwa kujiunga na EAC na sasa tuna ziada ya watu milioni 15 ambao watakaokuja kuwa wanachama wa hii familia kubwa,” amesema Rais Ruto.

Nchi nyingine wanachama wa EAC ni Tanzania, Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda, Demokrasia ya Congo na Sudan Kusini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!