Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Majeshi ya Urusi yadai kuua majenerali Ukraine
Kimataifa

Majeshi ya Urusi yadai kuua majenerali Ukraine

Spread the love

JESHI la Urusi lililopo katika operesheni maalum nchini Ukraine limedai kuwaua majenerali wawili katika shambulizi la mapema wiki hii. Anaripoti Joseph Nyoni kwa msaada wa mitandao…(endelea).

Gazeti la The Moscow Times limeeleza kuwa, pamoja na kuwaua majenerali hao, majeshi ya Urusi pia yamedai kuwaua maafisa 50 wa jeshi la Ukraine.

Hali hiyo imeelezwa kuwa inaendelea kuipa mtihani Ukraine, nchi ambayo imekuwa ikielemewa na mashambulizi makali kutoka kwa majeshi ya Urusi huku majenerali na maafisa wake wakubwa wa jeshi wakizidi kupoteza maisha.

Shirika la habari la RIA liliripoti kwamba  majenerali hao pamoja na maafisa 50  wa jeshi la Ukraine waliuawa katika mji wa Mashariki wa Kramatorsk nchini Ukraine tarehe 27 Juni mwaka huu.

Moscow pia imeeleza kuwa jaribio uasi lililofanywa na Wagner Yevgeny Prigozhin nchini Urusi halitaathiri operesheni za Urusi nchini Ukraine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!