Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Michezo Mamdonga atambulisha ngumi yake mpya sabasaba
Michezo

Mamdonga atambulisha ngumi yake mpya sabasaba

Spread the love

BONDIA machachari nchini Karim Said maarufu ‘Mandonga Mtu kazi’ ametembelea banda la Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo na kutangaza ngumi mpya iitwayo “Kingugi” anayotarajia kuitumia kwenye mchezo wa marudiano na Bondia Daniel Wanyonyi kutoka Kenya.  Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Mandonga ametangaza ngumi hiyo leo tarehe 29 Juni 2023 kwenye maonesho ya 47 ya Kimataifa Sabasaba ambayo yanaendelea jijini Dar es Salaam katika viwanja vya Mwl. Julius Nyerere.

Mandonga ameishukuru Serikali kwa kusimamia vema michezo hatua iliyomfanya ajulikane kimataifa na kuhamasisha vijana kupenda michezo ili kuendesha maisha yao.

Akimkaribisha bondia Mandonga Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Maonesho hayo ya 2023, Zahara Guga amesema Wizara ni mlezi wa masuala ya Utamaduni, Sanaa na Michezo. Hivyo, Mandonga ni miongoni mwa Wadau wake yupo kwenye ofisi yake ya kazi.

Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo imejikita kutoa huduma kwa wananchi na wadau wa sekta ya Utamaduni, Sanaa na Michezo na kuhamasisha wadau hao kurasimisha kazi zao ambazo ni ajira ya kujipatia kipato kwa kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Meridianbet yaibukia Tandika, yafungua duka jipya

Spread the love BAADA ya kupita maeneo mbalimbali hatimae kampuni yaMeridianbet imeibukia...

BiasharaMichezo

Ukiwa na Meridianbet ni rahisi kuwa milionea

Spread the love  CARABAO Cup raundi ya 3 Uingereza inaendelea na mechi...

Michezo

Jezi ya Samatta iliyoifunga Liverpool kuuzwa Genk

Spread the love  KLABU ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji imeamua kuanza...

BiasharaMichezo

Hii ndio historia ya El-Clasico, derby bora zaidi duniani

Spread the love  KILA nchi ina vilabu viwili hasimu na pinzani nje...

error: Content is protected !!