Tuesday , 30 May 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Korea washangilia bomu la Nyuklia
Kimataifa

Korea washangilia bomu la Nyuklia

Moja ya kombora la Korea Kaskazini baada ya kurushwa
Spread the love

KOREA Kaskazini imefanya sherehe kubwa kwa ajili ya kuwaenzi wanasayansi waliofanikisha majaribio makubwa ya bomu la Nyuklia nchini humo, anaandika Irene Emmanuel.

Sherehe hiyo imefanyika katika Mji Mmkuu, Pyongyang huku wananchi wakishangilia wanasayansi waliokuwa ndani ya basi katika barabara kuu za mji huo.

Wananchi walijumuika katika Uwanja wa Kim II-Sung yu kuwapongeza wanasayansi hao.
Siku ya Jumapili Korea Kaskazini ilifanyia jaribio kwa mafanikio bomu la Nyuklia aina ya Hydrogen lenye uwezo wa kufanya uharibifu.

Hili ni jaribio la sita kuhusu majaribio ya Nyuklia nchini humona kwamba lilisababisha mtetemeko wa ardhi wenye ukubwa wa 6.3 kwa kipimo cha rishta.

Korea Kaskazini imefanya jaribio hilo licha ya taharuki kutanda katika Peninsula ya Korea na vikwazo vya kila mara kutoka Marekani na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa dhidi yake.

Serikali ya Korea Kaskazini inasisitiza kuwa inalazimika kumiliki silaha za Nyuklia kwa lengo la kujihami kutokana na vitisho vya Marekani vya kuivamia kijeshi kwa mabomu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Mkutano wa Quad Hiroshima waibuka na kutafuta amani na ustawi wa Indo-Pacific

Spread the love  JITIHADA za mazungumzo ya Pande Nne (Quad), hazikuthaminiwa na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Kimataifa

Kiwango cha ukosefu wa ajira nchini China chaongezeka

Spread the love  WAKATI kiwango cha ukosefu wa ajira kwa vijana nchini...

Kimataifa

Kampuni za kigeni zahofia kuendelea na biashara China

Spread the love OPERESHENI ya kiuchunguzi inayofanywa na Serikali ya China kwa...

error: Content is protected !!