KESI dhidi ya rais wa zamani wa Marekani, Donald Trump kutokana na madai ya kujaribu kuingilia matokeo ya uchaguzi wa rais wa 2020 itaanza kusikilizwa Machi mwaka 2024 katika mahakama ya shirikisho jijini Washington nchini humo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).
Tarehe hiyo inatajwa kumuathiri kisiasa katika mbio zake za kuusaka urais wa taifa hilo kubwa duniani hasa ikizingatiwa itasikilizwa siku moja kabla ya uchaguzi wa ndani ya chama chake cha Republican wa kumchagua mgombea Urais.
Jana tarehe 28 Agosti 2023, Jaji Tanya Chutkan ambaye atasikiliza kesi hiyo amethibitisha itaanza tarehe 4 Machi 2024 siku moja kabla ya ‘Super Tuesday’, siku ambayo majimbo 15 hupiga kura za kuteua wagombea wa urais kwenye uchaguzi mkuu.
Takwimu zinaonyesha kwamba kufikia sasa Trump anaongoza miongoni mwa watu wanaonuia kuwania urais kupitia chama cha Repablikan.
Waendesha mashitaka walikuwa wamependekeza kesi hiyo ianze tarehe 2 Januari mwakani, wakati mawakili wa Trump wakiomba isogezwe hadi Aprili 2026, miaka miwili baada ya uchaguzi wa mwaka ujao kufanyika.
Hata hivyo, Jaji Chutkan alikataa mapendekezo hayo, wakati tarehe aliyotaja ikionekana kuathiri kampeni ya Trump, pamoja na kesi nyingi zinazomkabili.
Leave a comment