MADAI mapya ya ufisadi yaliyoibuliwa na Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, kwenye Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), hayawezi kumwacha salama, aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka hiyo, Mhandisi Deusdedit Kakoko.
Taarifa kutoka serikalini na TPA, zinasema karibu maeneo yote ambayo Rais Samia ameyagusia katika hotuba yake, hadi kuamua kuvunja bodi ya wakurugenzi ya mamlaka ya bandari, yalifanyiwa kazi wakati wa utawala wa Kakoko.
Kakoko ambaye alisimamishwa kazi na Rais Samia mwanzoni mwa mwaka huu, na kuchunguzwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).
Soma undani wa habari hii, katika Gazeti la Raia Mwema leo Jumanne, tarehe 7 Desemba 2021.
Leave a comment