Saturday , 11 May 2024
Home Habari Mchanganyiko JKT yawarejesha kambini vijana wa kujitolea
Habari Mchanganyiko

JKT yawarejesha kambini vijana wa kujitolea

Kaimu Mkuu wa Tawi la Utawala JKT, Kanali Hassan Mabena
Spread the love

 

MKUU wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Charles Mbuge, amewarejesha katika mafunzo, vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa kujitolea kwa mwaka 2020/2021. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Ni baada ya kurejeshwa nyumbani Februari 2021.

Akitoa taarifa hiyo leo Ijumaa, tarehe 30 Aprili 2021, jijini Dodoma, Kaimu Mkuu wa Tawi la Utawala JKT, Kanali Hassan Mabena amesema, vijana hao wanatakiwa kuripoti katika kambi walizokuwa wamepangiwa awali kuanzia tarehe 7-14 Mei 2021.

Amesema, vijana waliorejeshwa ni wale wenye elimu ya darasa la saba na kidato cha nne.

“Vijana wenye elimu ya kidato cha sita, ngazi ya cheti, stashahada, shahada na wale wenye taaluma ya uhandisi wataendelea kusubiri majumbani hadi hapo utaratibu mwingine utakapotangazwa,” amesema

Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limekuwa likiendesha mafunzo yakuwajengea uwezo vijana kwa kuwapa stadi za maisha ikiwa ni pamoja na uzalishaji mali, uzalendo, kilimo, ufugaji na kushiriki katika ujenzi wa Taifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC, Wizara ya Katiba wajadili uanzishaji haki binadamu katika biashara

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umefanya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Sitta ang’ang’ana wanafunzi watibiwe bure, Serikali yagoma

Spread the loveMBUNGE wa Urambo, Margaret Sitta, ameishauri Serikali iweke utaratibu wanafunzi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Waitara ahoji bungeni mwarobaini mauaji katika mgodi Barick North Mara

Spread the loveMBUNGE wa Tarime Vijijini (CCM), Mwita Waitara, ameitaka Serikali kutafuta...

error: Content is protected !!