Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Janeth Mbene apongeza HKMU, ataka wahitimu wajiajiri
Elimu

Janeth Mbene apongeza HKMU, ataka wahitimu wajiajiri

Spread the love

WAHITIMU wa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki (HKMU),  watakiwa kutumia elimu waliyoipata kufanya tafiti na kutatua changamoto mbalimbali zilizoko kwenye jamii. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Hayo yamesemwa leo chuoni hapo na aliyekuwa Naibu Waziri wa Fedha, janeth Mbele, wakati wa mjadala kuhusu masuala ya biashara na uchumi kuelekea mahafali ya 21 yanayofanyika kesho  Jumamosi chuoni hapo.

Alisema wanapomaliza Shahada au Stashahada kwenye udaktari uuguzi au ustawi wa jamii wasione wamefika mwisho na badala yake waendelee kutauta fursa zikiwemo za ujasiriamali.

Alisema vyuo vinatoa wahitimu wengi lakini soko la ajira ni dogo hivyo wanapaswa kuwa wabunifu kwa kutafuta mbinu za kujiajiri wenyewe na kuajiri wenzao kwa kutumia ujuzi walionao.

Naibu Waziri wa Fedha wa zamani, Janeth Mbene akimpa cheti mmoja wa wahitimu bora wa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki (HKMU), wakati wa kongamano lililofanyika jana chuoni hapo Mikocheni kuelekea mahafali ya 21 ya chuo hicho yanayofanyika kesho Jumamosi.

Alisema pamoja na changamoto za huduma za kiafya zinapaswa kuwa fursa kwa na kwenye changamoto nyingi ndiko kwenye fursa hivyo waaanzishe huduma za afya na kuanzisha biashara za huduma hizo.

“Wahitimu wawe wabunifu watoe suluhisho kwa changamoto hizo kwa kuanzisha shughuli mbalimbali ambazo zitaleta suluhisho na tatizo haliwezi kuwa mtaji kama wengine ambao wamekuwa wakitoa visingizo,” alisema

Aliwataka pia kujiendeleza kiteknolojia kwa kuanzisha huduma za kisasa ambazo mara nyingi huwa hazipatikani hasa maeneo ya vijijini hususan kwenye huduma za afya.

“Kama ni daktari, muuguzi unaweza kutumia ujuzi wako kwa kutumia teknolojia kuwahudumia wananchi walioko pale na uwe tayari kujituma kwasababu huduma hizi ni za wito isiwe tu ni ajira uwe na shauku ya kuwahudumia wananchi,” alisema

“Ndiyo maana wakati mwingine daktari au muuguzi anaitwa saa nane usiku anakwenda kuwahudumia wagonjwa kwasababu ana wito na kazi yake,” alisema

Janeth Mbele akifurahia zawadi aliyopewa na Makamu Mkuu wa HKMU, Profesa Yohana Mashalla kwenye kongamano la kitaaluma ambalo limefanyika chuoni hapo leo.

Mbene alikipongeza chuo cha HKMU kwa kuanzisha program atamizi kuwasaidia wahitimu kuanzisha na kuendeleza biashara zao badala ya kutegemea fani zao pekee.

Alisema wahitimu wanapaswa kutumia fursa zilizopo na washirikiane na wenzao kufanya jambo kwa pamoja kwani kwa kufanya hivyo wanaweza kuona matokeo mazuri mapema kuliko kila mtu kuwa kivyake vyake.

“Nimewapa changamoto wkenye amsuala ya ubunifu kwasababu kwenye mataifa mengi yaliyoendelea wahitimu wao wanakwenda kubuni vitu sasa na watanzania nao wafanye waache visingizo kwamba fursa ni chache watumie mazingira yaliyopo kutengeneza fursa,” alisema

Kuhusu mikopo ya elimu ya juu, Mbene aliitaka serikali kuwa makini na kuhakikisha wanaopewa mikopo hiyo ni wale wanaostahili kwani kumekuwa na malalamiko kwamba watu sahihi wanakosa na wanapewa watu wasiostahili.

Mgeni rasmi Janeth Mbene akifurahia moja ya bidhaa kwenye maonyesho yaliyofanyika kwenye kongamano hilo la HKMU.

“Haya malalamiko mmeyasikia kwa hiyo mimi ninachoweza kusema ni kwamba serikali iwe makini ili wanaopata wawe kweli wale wanaostahili kupata kwasabbau wakipata wenye uwezo inakuwa haina maana,” alisema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari Mchanganyiko

Ugawaji taulo za kike watajwa kutokomeza utoro shuleni

Spread the loveBAADHI ya wanafunzi na walimu wa shule za sekondari mkoani...

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

error: Content is protected !!