Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Israel yashambulia Lebanon, Gaza baada yakushambuliwa kwa roketi
Kimataifa

Israel yashambulia Lebanon, Gaza baada yakushambuliwa kwa roketi

Spread the love

 

JESHI la Israel limesema kuwa limeshambulia maeneo yenye uhusiano na kundi la wapiganaji wa Palestina Hamas ndani ya Lebanon na katika Ukanda wa Gaza. BBC imeripoti … (endelea).

Mashambulizi hayo yanakuja baada ya shambulio kubwa la roketi dhidi ya Israel kutoka Lebanon, ambalo Waisraeli walilaumu kundi la Hamas.

Jeshi la Ulinzi la Israel lilisema miundombinu ya “kigaidi” ya Hamas ilipigwa kusini mwa Lebanon.

Hali ya wasiwasi imetanda baada ya polisi wa Israel kuvamia msikiti wa Al-Aqsa mjini Jerusalem usiku mtawalia mapema wiki hii.

Msikiti huo ni eneo la tatu takatifu kwa Uislamu, na uvamizi wa Israel umezusha makabiliano makali na Wapalestina ndani na kusababisha hasira katika eneo hilo kubwa.

Mkuu wa Hamas Ismail Haniyeh, ambaye alikuwa Lebanon wakati roketi hizo ziliporushwa, alisema Wapalestina “hawataketi wakitazama tu” uvamizi wa Israel ukiendelea.

Katika taarifa mapema siku ya Ijumaa, IDF iliandika kwenye Twitter kwamba ilikuwa imejiwekea melenga ya mahali pa kushambilia “ikiwa ni pamoja na miundombinu ya kigaidi ya Hamas kusini mwa Lebanon”.

IDF iliongeza kuwa haitaruhusu Hamas kufanya kazi kutoka Lebanon na kushikilia Lebanon “kuwajibika kwa kila moto ulioelekezwa kutoka katika eneo lake”.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!