PICHA za hati za siri kutoka Pentagon na NATO juu ya utayarishaji wa shambulio la Ukraine dhidi ya Urusi zimevuja katika mitandao ya Twitter na Telegraph. Yameripoti Mashirika ya Kimataifa…(endelea).
Licha ya kuonekana kubadilishwa kiasi hati hizo zinaonekana kuwa za kweli kulingana na gazeti la New York Times, likinukuu vyanzo visivyojulikana katika utawala wa Biden.
Tarehe za hati hizo ilikuwa Machi Mosi , hivyobasi inakisiwa kwamba huenda mipango inaweza kuwa ilibadilika tangu wakati huo.
Hata hivyo hazitaji eneo au mahala pa mashambulizi hayo.
Lakini zina habari kuhusu brigedi ngapi Ukraine inapanga kujiandaa kwa shambulio hilo na ni vifaa gani watapata na kutumia wakati huo. Pia wana taarifa kama vile matumizi ya kila siku ya risasi kwa HIMARS.
Ukweli kwamba nyaraka zingeweza kubadilishwa unathibitishwa na ukweli kwamba kwenye moja ya hati hizo, hasara iliopata wanajeshi wa Urusi inakadiriwa kufikia kati ya 16-17,000, huku Ukraine ikiwa 71.5 elfu, kwa mujibu wa gazeti hilo.
Warusi kati ya 16-17, 000 na waukraine 71,500? Duh!
Zile ndege za F-16 zinaogopa makombora ya supersonic? Duh!