Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Muhongo ampa tano Rais Samia
Habari za Siasa

Prof. Muhongo ampa tano Rais Samia

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

MBUNGE wa Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo, ameipongeza Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa fedha kiasi cha Sh. 4.75 bilioni, kwa ajili ya usambazaji maji katika kata mbili zilizokuwa zimeachwa katika mradi wa Maji ya Boma la Mugango-Kiabakari-Butiama. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mara … (endelea).

Pongezi hizo zimetolewa na tarehe 6 Aprili 2023 na Prof. Muhongo, kupitia taarifa iliyotolewa na Ofisi yake ya Jimbo la Musoma Vijijini.

“Tunaanza kwa kutoa shukrani nyingi sana kwa Serikali yetu inayoongozwa vizuri na Rais wetu, Dk. Samia. Kata mbili zilizokuwa zimeachwa kwenye mradi wa Sh. 71.5 bilioni wa maji sasa zimepatiwa fedha za kujengewa miundombinu ya usambazaji wa maji kwenye kata hizo , hii ni zawadi ya Pasaka,” imesema taarifa hiyo.

Kupitia taarifa hiyo, Prof. Muhongo amesema wananchi waishio kwenye chanzo cha maji katika Kata ya Mugango na Tegeruka, watapata maji kupitia bomba hilo.

“Mkandarasi wa mradi huu wa kata mbili ameshapatikana na taratibu zote zimekamilika, kifuatacho ni utiaji saini, hafla itakayofanyika kijijini Mayani, Kata ya Tegeruka, tarehe 12 Aprili 2023. Viongozi mbalimbali wa chama na Serikali watakuwepo,” imesema taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!