KAMATI ya Sheria na hadhi ya Wachezaji inatarajia kutoa maamuzi juu ya kesi ya kimkataba kati ya mchezaji Benard Morrison na uongozi wa klabu ya Yanga, baada ya shauli hilo kusikilizwa kwa siku tatu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Elias Mwanjala jana Jumanne alieleza kuwa sakata hilo litatolewa maamuzi leo baada ya pande zote mbili kutakiwa kuwasilisha nyaraka ambazo ni muhimu na baadae kutoa hukumu.
“Kuna nyaraka moja ambayo haijakamilika na tunategemea kuipata kesho (leo) saa nne asubuhi tunaanza kikao na baadae kutoa uwamuzi, hapa tulipofika ni pazuri, msiwe na shaka muwe na subira,” alisema Mwanjala.
Mchezaji huyo ambaye Jumamosi alitambulishwa na klabu ya Simba licha ya klabu ya Yanga kudai kuwa Morrison bado anamkataba na klabu hiyo na kesi yao bado ipo kwenye Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) chini ya kamati ya Sheria.
Morrison alifika nchini 15 January, 2020 na kujiunga na klabu ya Yanga katika dirisha dogo la usajili kwa mkataba wa miezi sita, licha ya baadae Yanga kudai kuwa klabu hiyo ilimuongeza mkataba wa miaka miwili.
Kwa nn yanga hawana shukuran kumtaka mchezaji kwa kumfungulia kesi na nikwa nn iwe hvyo?