Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amemteua Dk. Immaculate Sware Semesi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC). Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Kabla ya uteuzi huu Dk. Semesi alikuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Uhifadhi wa Bahari na Maeneo Tengefu na anachukua nafasi ya Dk. Samuel Gwamaka Mafwenga ambaye amemaliza muda wake.
Taarifa iliyotolewa leo Ijumaa na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Zuhura Yunus imesema uteuzi huo umeanza tarehe 5 Januari 2024.
Dk. Semesi awali alikuwa kada wa Chadema na kuteuliwa na chama hicho kuwa Mbunge wa viti maalumu kuanzia mwaka 2015 hadi 2020.
Aidha, Juni 2020 Dk. Semesi (Kilimanjaro ), na wabunge wenzie wawili Anna Gidarya (Manyara ) na Latifa Chande (Lindi) waltangaza kuachana na CHADEMA na kuomba kujiunga na CCM wakisema wamejionea kwa macho yao kazi iliyofanywa na serikali ya awamu ya tano wakati huo ikiwa chini ya Hayati Rais John Magufuli.
Leave a comment