Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa DC Rufiji atahadharisha mafuriko kuongezeka, ACT wataka wananchi wafidiwe
Habari za SiasaTangulizi

DC Rufiji atahadharisha mafuriko kuongezeka, ACT wataka wananchi wafidiwe

Spread the love

MKUU wa Wilaya ya Rufiji, Meja Edward Gowele ametoa tahadhari kwa wananchi wanaoishi karibu na maeneo yalliyokumbwa na mafuriko ya maji yaliyofunguliwa kutoka kwenye Bwawa la Mwalimu Nyerere wahame kwa kuwa bado yanaendelea kufunguliwa. Anaripoti Faki Ubwa, Pwani … (endelea).

Akizungumza na MwanaHALISI Online leo Jumapili kwa njia ya simu, Gowele  amesema ili kuokoa mradi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere ni lazima maji yapunguzwe yawe katika kiwango kinachohitajika.

“Tumeambiwa tuwe na tahadhari  kwa wananchi wanaoishi mabondeni kwani Bwawa la Mwalimu Nyerere linaendelea kufunguliwa ili kuokoa mradi huu.”

Kuhusu taarifa ya kiwango cha maji kitachofunguliwa amesema kitakuwa ni zaidi ya lita milioni 7.

DC Gowele amesita kufafanua zaidi na kusisitiza kuwa hayo ni masuala la kitaam hivyo hawezi kukisia.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo, Isihaka Mchinjita aliyekwenda Rufiji jana Jumamosi katika eneo lenye maafa, amesema hali ni mbaya na kwamba Serikali onatakiwa itoe taarifa ya maafa kwa umma ili watu Watanzania wajue kinachoendelea.

DC Rufiji

Mchinjita ambaye pia ni Waziri Mkuu Kivuli wa Baraza la Mawaziri Vivuli la Chama hicho ameitaka Serikali kuwafidia wananchi walioathirika na maafa hayo yaliyosababishwa na kufunguliwa na kwa Bwawa la Mwalimu Nyerere.

1 Comment

  • Mchinjita wa ACT Wazalendo, unaongea ili usikike kama mpinzani mjinga. Bila bwawa la Nyerere maafa yangezidi. Wananchi walitangaziwa na wametangaziwa. Mabondeni waondoke. Wametangaziwa tena. Siasa zako zingependeza ungeendelea kutangazia na kuwaelisha watu. Haya ni mafuriko yanayadhibitiwa, na mradi bado unaendelea kujengwa.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!