Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge: Wabunge Tanzania wanalipa kodi
Habari za Siasa

Bunge: Wabunge Tanzania wanalipa kodi

Bunge la Tanzania
Spread the love

 

OFISI ya Bunge la Tanzania imesema, wabunge kama ilivyo kwa watumishi wengine wa umma na viongozi wa kisiasa nchini humo, wanakatwa kodi zote stahiki kwa mujibu wa sheria. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Miongoni mwa kodi hizo ni kodi ya mapato (PAYE), inayokatwa kwenye mishahara ya wabunge ya kila mwezi.

Taarifa ya Kitengo cha Mawasiliano na Uhisiano wa Kimataifa ya Bunge la Tanzania, iliyotolewa leo Jumanne, tarehe 3 Agosti 2021, imesema kinachoendelea kitandaoni kwamba wabunge hawalipi kodi kwenye mishahara hao hakina ukweli.

Ofisi hiyo ya Bunge, imetoa ufafanuzi huo baada ya siku za hivi karibuni, kuibuka taarifa mitandaoni kwamba, wabunge hawalipi kodi hivyo maumivu wanayoyapata kupitia tozo za miamala ya simu hawahusiki nayo.

Tozo hizo, zilianza kutumika tarehe 15 Julai 2021, baada ya kupitishwa na Bunge. Tozo hizo zimekuwa zikilalamikiwa na wananchi kwamba zinawaumiza na tayari Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameagiza zipitiwe upya kuangalia kama zinaweza kupunguzwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!