Sunday , 2 April 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Biashara za Saudia, Emirates, Bahrain, Misri zazuiwa Qatar
Kimataifa

Biashara za Saudia, Emirates, Bahrain, Misri zazuiwa Qatar

Spread the love

MGOGORO wa Qatar na mataifa jirani unazidi kukua na sasa taifa hilo (Qatar) limezuia kuingizwa biashara kutoka Saudi Arabia, Emirates, Bahrain na Misri. Anaandika Faki Sosi … (endelea).

Sheikh Ahmed Jassem bin Mohammed Al Thani ambaye ni Waziri wa Uchumi na Biashara wa Qatar ameagiza sekta zote nchini humo kuacha kuagiza na kununua bidhaa yoyote inayotoka miongoni mwa nchi hizo.

Waziri huyo amesema kuwa, serikali itaendesha msako ili kujiridhisha kama agizo hilo limetekelezwa sana na namna lilivyokusudiwa na kwamba, atakayebainika kukiuka, hatua kali zitachukuliwa dhidi yake.

Serikali ya Qatar imeeleza kushinda vikwazo vya awali vilivyowekwa Bahrain, Saudia, Emirates na Misri.

Juni mwaka jana Bahrain, Saudi, Bahrain, Emirates na Misriziliitenga Qatar kwa madai kusaidia ugaidi jambo lililoenda sambamba na kufunga mipaka yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Marekani yatia mguu maaandamano Kenya, yatoa maagizo kwa Rais Ruto, Odinga

Spread the love  Mabalozi kutoka nchi sita za Magharibi, zikiongozwa na Marekani,...

Kimataifa

Papa Francis alazwa hospitali kutokana na maambukizi ya mapafu

Spread the love  KIONGOZI wa Kanisa katoliki duniani, Papa Francis jana Jumatano...

Kimataifa

Nyumba ya babu yake Makamu wa Rais wa Marekani yatafutwa Zambia

Spread the love  KAMALA Harris, makamu wa rais wa Marekani, amepanga kutembelea...

Kimataifa

Benki ya Uswizi mbioni kuziwekea vikwazo akaunti za siri za Wachina

Spread the love  WAKATI Serikali na Benki ya Uswizi ikichukua hatua kali...

error: Content is protected !!