Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Benki ya Dunia yatoa somo kwa Regrow
Habari Mchanganyiko

Benki ya Dunia yatoa somo kwa Regrow

Spread the love

 

WATAALAM kutoka Benki ya Dunia wanaendesha semina kwa Wataalam wanao simamia utekelezaji wa Mradi wa Kuboresha Usimamizi wa Maliasili na Kukuza Utalii Kusini mwa Tanzania (REGROW) juu ya mfumo wa upokeaji na kushughulikia malalamiko pale yanapotokea wakati wa utekelezaji wa mradi. Anaripoti Yusuph Kayanda, Morogoro … (endelea).

Akifungua Mafunzo hayo Mkoani Morogoro, Mkurugenzi wa Kitengo cha Utafiti na Mafunzo, Dk. Edward Kohi ameipongeza Benki ya Dunia kwa kuandaa Mafunzo hayo ambayo yataimarisha zoezi zima la upokeaji wa malalamiko na namna ya kuyashughulikia kwa wakati ili malengo ya mradi yafikiwe kwa wakati.

Dk. Kohi ameongeza kuwa mfumo huo wa REGROW wa kupokea malalamiko ni muhimu kwakuwa unatoa nafasi kwa wananchi na wadau mbalimbali kutoa malalamiko au maoni yenye nia ya kuboresha zoezi zima la utekelezaji wa mradi kwa njia shirikishi.

Aidha ametoa wito kwa washiriki kuzingatia Mafunzo hayo ili kupata uelewa mpana wa kughulikia malalamiko si kwa mradi tu wa REGROW bali kwenye kazi za kilasiku za Wizara ya Maliasili na Utalii.

Wakizungumzia mafunzo hayo ya siku mbili, Maafisa Wandamizi wa Maendeleo ya Jamii Benki ya Dunia, Roselyn Kaihula na Bi. Annette Omolo, wamesema mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo wataalam wanotekelezaji mradi wa REGROW, namna ya kushughulikia malalamiko na changamoto mbalimbali kwa ufanisi zaidi hali itakayo pelekea zaidi kufikiwa kwa malengo kusudiwa ya mdari huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

Habari Mchanganyiko

Tanzania  yasisitiza kuwa Kituo Kikuu cha Uchimbaji Madini Afrika

Spread the loveTanzania imeendelea kusisitiza adhma yake ya kuwa kituo kikuu cha...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

error: Content is protected !!