Wednesday , 8 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Basi lateketeza maisha ya watu 50
Kimataifa

Basi lateketeza maisha ya watu 50

Spread the love

BASI la abiria lililokuwa likitokea jijini Nairobi kuelekea Kisumu nchini Kenya, limepata ajali na kuua watu takribani 50. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Ajali hiyo imetokea leo Jumatano alfajiri ya tarehe 10 Oktoba 2018, katika barabara ya Londiani-Muhuroni, Kaunti ya Kericho.

Basi lililopata ajali linamlikiwa na kampuni ya Western Express Sacco Limited.

Kamanda wa Polisi Kaunti ya Kericho, James Mogera amethibitisha kutokea kwa ajili hiyo na kuongeza, “miongoni mwa waliokutwa na mauti, ni watoto nane walio chini ya umri wa miaka mitano.”

Amesema, majeruhi waliokuwa katika basi hilo lenye uwezo wa kubeba abiria 67, wamepelekwa katika Zahanati ya Fort Ternan na Hospitali ya Kaunti ya Muhoroni Sub kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Chanzo cha ajali hiyo kinadaiwa kuwa basi kuvamia reli kisha kupanda katika shamba la mawe na kuanguka chini mita 20.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!